Psalms 51:1-3

Kuomba Msamaha

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi. Baada Ya Kukemewa Na Nabii Nathani Kwa Kuzini Na Bathsheba)


1 aEe Mungu, unihurumie,
kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,
kwa kadiri ya huruma yako kuu,
uyafute makosa yangu.

2 bUnioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.


3 cKwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
Copyright information for SwhKC